Comments

Wanachuo Iran walaani kuvunjiwa heshima Mtume SAW

Maelfu ya wanafunzi na wanazuoni wa Vyuo Vikuu Vya Kiislamu Katika mji wa Qum, Iran wamefanya maandamano makubwa wakipinga kitendo cha gazeti la Charlie Hebdo la nchini Ufaransa kuchapisha vikatuni vya kumvunjia heshima Mtukufu Mtume Muhammad (SAW). 

Maandamano hayo yaliyofanyika katika chuo cha Faidhiya cha mjini Qum, yamewashirikisha wanafunzi , wahadhiri na wanazuoni kutoka nchi mbalimbali za dunia kulaani kitendo hicho cha kumvunjiwa heshima Mtukufu Mtume (SAW). 

Katika maandamano hayo, waandamanaji walitoa nara za kulaani gazeti hilo kwa hatua ya kuthubutu kuchezea hisia za Waislamu zaidi ya bilioni mbili duniani. Hujjatul-Islam Wal-Muslimin, Sayyid Muhammad Saidi, ambaye pia ni msimamizi wa Haram ya Bibi Fatima Maasumah, kwa kusema: 

"Maadui wa Uislamu wamefuata mkondo huo baada ya wao kushindwa kuzima nuru ya Mwenyezi Mungu yaani Uislamu na kwamba hiyo ni juhudi iliyofeli." Jana pia maelfu ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Iran waliandamana mbele ya Ubalozi wa Ufaransa mjini Tehran kulaani hatua ya gazeti la Charlie Hebdo kuchapisha tena vibonzo vinavyomvunjia heshima Mtume wa Uislamu Muhammad (SAW).
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

New Hope Company. Powered by Blogger.

Facebook

Wazo Hai

Search This Blog

Blog Archive

Flickr

Social Share

Featured
Featured

Labels

Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

TANGAZA NASI HAPA

East Africa Radio Live Here

Tags

Fashion

Sponsor

Videos