Comments

Obama alaani mauaji ya mateka wa Japan



Rais wa Marekani Barack Obama amelaani kile alichokitaja kuwa mauaji ya kikatili ya mmoja wa raia wa Japan aliyekuwa akishikiliwa mateka na wanamgambo wa Islamic State Haruna Yukawa.

Rais Obama pia alitaka mateka mwingine anayeshikiliwa na wanamgambo hao mwandishi wa habari Kenji Goto kuachiliwa mara moja

Kwa njia ya video Goto alionekana kwenye mitandao akishika mkononi picha ya maiti ya bwan Yukawa.

Mapema wataalamu mjini Tokyo na Marekani walisema kuwa wanatathmini ukweli wa picha hiyo.

Waziri mkuu nchini Japan Shinzo Abe alisema kuwa ameghadhabishwa na video hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

New Hope Company. Powered by Blogger.

Facebook

Wazo Hai

Search This Blog

Blog Archive

Flickr

Social Share

Featured
Featured

Labels

Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

TANGAZA NASI HAPA

East Africa Radio Live Here

Tags

Fashion

Sponsor

Videos