Comments

iPhone 6 ya dhahabu yenye thamani ya shilingi milioni 3.8 Yamliza Mtangazaji wa Times FM

Mtangazaji wa kipindi cha The Switch cha Times FM, Cnda King ameporwa simu ya thamani kubwa ya iPhone 6 yenye dhahabu (24 karat gold plate).
Cnda ambaye pia ataanza kuonekana kwenye kipindi kipya cha TV kiitwacho 10 Made in Africa, ameimbia Bongo5 kuwa simu hiyo iliporwa jana Jumapili (March 1) akiwa kwenye taa za traffic maeneo ya Kamata, Kariakoo wakati akitokea airport mida ya saa mbili na nusu usiku.


iPhone 6 iliyozungushiwa dhahabu

“Nilikuwa kwenye mataa nasubiri taa ziruhusu magari kwenda huku nikichat,” amesema Cnda. “Kioo kilikuwa chini, akatokea jamaa na kunipora na kukimbia,” ameongeza mtangazaji huyo.

Cnda amesema gharama ya simu hiyo ukijumlisha na dhahabu zilizowekwa nyuma ya simu hiyo ni shilingi milioni 3.8.

“Niliinunua November last year ikiwa kawaida ila niliipeleka Hong Kong February mwaka huu ikawe pimped na hiyo 24 karat gold plate.”

Cnda hajaacha kuwaonya watumiaji wa simu kuepuka kuchat wakiwa kwenye foleni hasa katika maeneo yenye watu wengi.

“Watu wawe makini sana na hawa jamaa barabarani,” amesisitiza.



“Ukiacha kukuibia wanaweza kukuumiza pia.”
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

New Hope Company. Powered by Blogger.

Facebook

Wazo Hai

Search This Blog

Blog Archive

Flickr

Social Share

Featured
Featured

Labels

Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

TANGAZA NASI HAPA

East Africa Radio Live Here

Tags

Fashion

Sponsor

Videos