Comments

Watu 42 wamepoteza maisha na wengine 82 kujeruhiwa baada ya mvua ya upepo mkali kunyesha mkoani Shinyanga.

Watu 42 wamepoteza maisha na wengine 82 kujeruhiwa baada ya mvua ya upepo mkali kusababisha mafuriko katika kata ya
mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga.


Mvua hiyo ambayo ilinyesha kwa muda mfupi imewaacha watu 3,500 bila makazi katika kaya 350 huku nyumba zikifurika maji na baadhi ya mifugo ikisombwa.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bw. Ali Nasoro Rufunga amesema mvua hiyo ya mawe iliyoambatana na upepo mkali ilisababisha mafuruko katika kata ya Mwakata kuezua nyumba na nyingine kuanguka.

Amesema mali mbalimbali zimeharibiwa vibaya ikiwemo mifugo kuzolewa na maji na vyakula kwenye eneo lote lililokumbwa na mafuriko hayo.

Hali ya majeruhi ambao wamepelekwa katika hospitali mbalimbali bado sio nzuri kwa baadhi ingawa wengine wanaendelea vizuri.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

New Hope Company. Powered by Blogger.

Facebook

Wazo Hai

Search This Blog

Blog Archive

Flickr

Social Share

Featured
Featured

Labels

Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

TANGAZA NASI HAPA

East Africa Radio Live Here

Tags

Fashion

Sponsor

Videos