Comments

Diamond na Davido Ndo Basi Tena!?

 https://www.facebook.com/
Diamond na Davido wana beef? Hili ni swali ambalo watu wengi bado hawajapata jibu lake hasa baada ya wiki hii Davido kutweet maneno yaliyohisiwa kuwa yanamlenga Diamond. 

Akizungumza kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa hii, meneja wa Diamond, Babu Tale amesema Diamond na Davido sio washkaji ila wana mahusiano ya kibiashara tu.

“Hakuna vita mimi na menejimenti ya Davido, Tunaongea,” amesema Tale.

“Hapa ninaweza nikakuonesha meseji za mimi na Kamala ambaye ni meneja wa Davido. Nikinukuu maneno ya Kamala kwangu ile meseji ambayo Davido aliposti ya kwanza hakuwa anamface Diamond according to Kamala. Akaniambia mbona ‘watanzania wameelewa vibaya’ nikamwambia ‘tuliache hili limepita na limeshatokea hatuwezi kuwaambia bana Davido hajaongea hivi kwa maana hii, tutafute njia nyingine ambayo Davido anaweza akasehewa na Watanzania,” ameongeza Tale.

“Lakini sitaki kuamini kama Davido na Diamond wana vita. Juzi Davido alikuwa anaposti vitu vyake sio kwa sababu ya Diamond. Watanzania wote washaanza kusema ‘oooh Davido ashaanza kumtukana Diamond’. Nikwambie kitu kimoja Diamond hata baada ya kufanya ile video huwaga hawachati, Diamond akimtaka Davido ataniambia mimi au atamwambia Salam au Kamala.”
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

New Hope Company. Powered by Blogger.

Facebook

Wazo Hai

Search This Blog

Blog Archive

Flickr

Social Share

Featured
Featured

Labels

Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

TANGAZA NASI HAPA

East Africa Radio Live Here

Tags

Fashion

Sponsor

Videos